NITAOA NIKIFIKA THELATHINI

NITAOA NIKIFIKA THELATHINI

Si kama nataka kufa, kwa haya nitokwambia
Ila nofia kujuta, pindi yakikutokea
Nogopa  nafsi nisuta, mjomba nsipokwambia
             Nitaoa nikifika thelathini

Natambua nia yako, nia unopigania
Sikukwacha peke yako, pekee kiteketea
Shikamana na wenzako, usia me nakwambia
              Nitaoa nikifika thelathini.

Nataka kupa wosia, li kazi uufanyie
Sio uje puuzia, sitajilaumu mie
Kidogo hebu sikia, kisha ukazingatie
            Nitaoa nikifika thelathini.

Wangindo mi nawajua, na hasa nawatambua
Kidogo kifanikiwa, haraka taka kuoa
Mjomba we zingatia, usi harakie ndoa
            Nitaoa nikifika thelathini.

Kama ukipata kazi, tulia kwa kujipanga
Usijivishe li vazi, kabla maisha kujenga
Tena ipo wazi wazi, kuoa ni kujifunga
           Nitaoa nikifika thelathini.

Misingi ikisimama, hapa hakuna utata
Usimuulize mama, ila shauri we kata
Kuoa ni jambo jema, ila maisha kipata
         Nitaoa nikifika thelathini.

Tena sipende umimi, ukoo kuurithia
Yako yaweke moyoni, na mengine puuzia
Hutobaki masikini, labda apende jalia
          Nitaoa nikifika thelathini.

Ukioa thelathini, si kwamba umechelewa
Iweke tu akilini, watoto taka lelewa
Mke utampa nini, kama hujajaaliwa
          Nitaoa nikifika thelathini.

Nataka kusema mengi, ila utapuuzia
Ukayatoa msingi, kwa mbali kuyatupia
Mke anataka mengi, mjomba we zingatia
       . .nitaoa nikifika thelathini.

BAHARI/ Kibwagizo/ kiitikio:

Sijui niseme nini, kama sio mesikia
Nitaweka akilini, le yote lo niambia
Nitaoa thelathini, mjomba mi nakwambia
       Nitaoa nikijipanga
       Nitaoa nikijenga
       Nitaoa nikipenda
       Nitaoa nikifika thelathini

Comments

Popular posts from this blog

SHULE ZENYE ADA KUBWA ZAIDI TANZANIA

STOP SHARING

RAFIKI WA KWELI