Posts

Showing posts from October, 2018

TANZANIA SHOTOKAN KARATE TOURNAMENT

Image
This year in Dar es salaam

NITAOA NIKIFIKA THELATHINI

NITAOA NIKIFIKA THELATHINI Si kama nataka kufa, kwa haya nitokwambia Ila nofia kujuta, pindi yakikutokea Nogopa  nafsi nisuta, mjomba nsipokwambia              Nitaoa nikifika thelathini Natambua nia yako, nia unopigania Sikukwacha peke yako, pekee kiteketea Shikamana na wenzako, usia me nakwambia               Nitaoa nikifika thelathini. Nataka kupa wosia, li kazi uufanyie Sio uje puuzia, sitajilaumu mie Kidogo hebu sikia, kisha ukazingatie             Nitaoa nikifika thelathini. Wangindo mi nawajua, na hasa nawatambua Kidogo kifanikiwa, haraka taka kuoa Mjomba we zingatia, usi harakie ndoa             Nitaoa nikifika thelathini. Kama ukipata kazi, tulia kwa kujipanga Usijivishe li vazi, kabla maisha kujenga Tena ipo wazi wazi, kuo...